Jumatano, 28 Desemba 2016

Dhamana ya Mbunge Lema yagonga mwamba

Mbunge wa Arusha mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema amekosa dhamana baada ya mawakili wa upande wa Jamhuri kuweka pingamizi kukata rufaa.

Mawakili wa Godbless walikusudia leo Dessemba 28, kuwasilisha hoja sita mahakamani kwa kusudio la kutaka mteja wao apewe dhamana, lakini hali imekuwa tofauti baada ya Jamhuri kupinga rufaa hiyo.

Lema alikamatwa Novemba 2 mjini Dodoma, tangu wakati huo, ameshikiliwa katika gereza kuu la Kisongo jijini Arusha ambako amekaa kwa siku 56 sasa.

Baada ya kukamatwa mbunge huyo alifikishwa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, bwana Lema alipata dhamana na hakimu mkazi Desdery Kamugisha katika kesi namba 440 na 441/2016 akidaiwa kutoa lugha za uchochezi dhidi ya raisi wa awamu ya tano John Pombe Magufuli.

Cristiano Ronaldo ameshinda tuzo ya 9 kwa 2016

Mwanasoka wa wa kimataifa, Cristiano Ronaldo wa nchi ya Ureno, ambaye anachezea klabu ya mpira ya Raal Madrid ya Hispania anakamilsha mwaka wa 2016 kwa kushinda tuzo yake ya tisa.
Bwana Cristiano alifanikiwa  kushinda tuzo hiyo iliyojulikana kama Globe Soccer Award hapo Dubai.

Tuzo hii ya mkata kabumbu bora wa dunia (Globe Soccer Award) kwa mwaka huu wa 2016 imekuwa ni tuzo ya 9 kwa Cristiano kwa mwaka huu wa 2016, hii ni baada ya kujishindia tuzo kadha wa kadha, ikiwamo, The World Soccer Award, Four Four Two, Espy, Di Stéfano Award, Goal.com, FIFA Club Golden Ball, na Ballon d'Or.

Katika tuzo hiyo ya Globe Soccer Award 2016 aliyoibuka Ronaldo mshindi ilikuwa pia ikiwania na wachezaji kama Lionel Messi, Gonzalo Higuan, Antonie Griezmann, Jamie Vardy, mwanasoka huyu ameweza kushinda tuzo hizo kwa mara ya nne sasa, hii ni miaka tofauti ambayo amewvza pia kushinda tuzo hizi 2011, 2013 na 2014.

Hoja sita za Mbunge Godbles Lema kusikilizwa leo

Hoja sita za mawakili wa mbunge wa Arusha mjini (Chadema), Godbles Mlema kupinga kunyimwa dhamana zinatarajiwa kusikilizwa leo mbele ya mahakama kuu jijini Arusha.
Wakili Sheck Mfinanga anayemwakilisha Lema alisema waliwasilisha hoja hizo za rufaa kupinga uamuzi wa kunyimwa dhamana mteja wao.

Mbunge Lema anashikiliwa katika gereza kuu la Kisongo jijini Arusha tangu akamatwe Novemba 2 mwaka huu mjini Dodoma. Na sasa amekaa siku kwa 56.

Mara baada ya ya kukamatwa na kufikishwa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, Lema alipewa dhamana na hakimu mkazi Desdery Kamughisha katika kesi namba 140 na141/ 2016 akidaiwa kutoa kauli za uchochezi dhidi ya raisi John Pombe Magufuli.

Hata hivyo, mkurugenzi wa mashitaka DPP alikata rufaa ya kupinga uamuzi wa mahakama kumpa dhamana Godbles Lema.

Hali imepelekea mawakili wa Lema nao kukata rufaa ya kupinga mteja wao kunyimwa dhamna, ili kesi isikilizwe tena leo baada ya kukwama kwa mda mrefu kutokana na kuwapo pingamizi nyingi za kisheria zilizowasilishwa na upande wa pili wa kesi (Jamhuri).










Jumamosi, 3 Desemba 2016

Baada ya Uchaguzi nchini Gambia, Barrow asema..

Baada ya uchaguzi nchini Gambia, raisi mteule wa nchi hiyo Bwana Adam Barrow amesema kuwa ni wakati wa kujenga Ghana yenye matumaini mpya.
Adama Barrow mwenye umri wa  miaka 51, na ambaye ni tajiri anayejishughulisha na biashara ya kujenga na kuuza majengo(nyumba), ameweza kushinda baada ya matokeo kutangazwa siku ya ijumaa na mkuu wa tume ya uchaguzi nchini Gambia, , Alieu Momarr Njai.

Barrow amemzidi Yahya kwa kura 51,416, ambapo kura za Barrow zilikuwa ni 263,515(45.5%) na Yahya kupata kura 212,099(36.7).

Raisi anayeachia madaraka nchini humo bwana Yaya Jammeh amekiri kushindwa, hii ni baada ya kumpigia Barrow na kumwahidi kumsaidia kujenga Gambia.


Yaya Jammeh ameweza kuingoza Gambia kwa miaka takribani 22, ambapo aliichukua nchi kwa mabavu na kujisimikia uongozi wa juu wa nchi ya Gambia(raisi).

Uchaguzi wa Gambia umewaacha wengi midomo wazi baada ya ushindi wa bwana Barrow kwa kile ambacho hakikutarajiwa, kwani Adam Barrow ni mgeni katika siasa na kwa upande wa Jammeh naye amekiri kushindwa jambo ambalo ni nadra kwa kiongozi mwenye tabia za kidikteta(mabavu).