Jumanne, 31 Januari 2017

Tazama matokeo ya kidato cha nne 2016 kwa urahisi na kasi sana

Bonyeza link hapo chini...
KAAGYA SEC. SCHOOL - S2161 KIBASUKA SEC. SCHOOL - S2288 KIPUMBWI SEC. SCHOOL - S4304
KABAGWE SEC. SCHOOL - S2156 KIBATA SEC. SCHOOL - S2576 KIRACHI SEC. SCHOOL - S2855
KABALE SEC. SCHOOL - S0871 KIBAYA SEC. SCHOOL - S5023 KIRAENI GIRLS SEC. SCHOOL - S0207
KABALE-BARIADI SEC. SCHOOL - S1723 KIBEDYA SEC. SCHOOL - S3842 KIRANDO SEC. SCHOOL - S4785
KABANGA SEC. SCHOOL - S0611 KIBELE SEC. SCHOOL CENTRE - P3909 KIRANDO SEC. SCHOOL CENTRE - P4785
KABANGA SEC. SCHOOL CENTRE - P0611 KIBELE SEC. SCHOOL - S3909 KIRANGARE SEC. SCHOOL - S0615
KABASA SEC. SCHOOL - S1477 KIBENGU SEC. SCHOOL - S0659 KIRANJERANJE SEC. SCHOOL - S2573
KABILA SEC. SCHOOL - S1444 KIBEREGE SEC. SCHOOL - S1747 KIRANYI SEC. SCHOOL - S1864
KABIRIZI SEC. SCHOOL - S3267 KIBETA SEC. SCHOOL - S4327 KIRARE SEC. SCHOOL - S5063
KABITA SEC. SCHOOL - S1704 KIBIMBA SEC. SCHOOL - S3162 KIRETI SEC. SCHOOL - S2953
KABUGARO SEC. SCHOOL - S2709 KIBINDU SEC. SCHOOL - S3177 KIRIBA SEC. SCHOOL - S2076
KABUHORO SEC. SCHOOL - S3032 KIBIRASHI SEC. SCHOOL - S2389 KIRIKI SEC. SCHOOL - S0468
KABUKU SEC. SCHOOL - S0714 KIBIRIZI SEC. SCHOOL - S3290 KIRIKI SEC. SCHOOL CENTRE - P0468
KABUKU SEC. SCHOOL CENTRE - P0714 KIBITI SEC. SCHOOL CENTRE - P0413 KIRIMA SEC. SCHOOL - S3672
KABULA SEC. SCHOOL - S2535 KIBO SEC. SCHOOL - S0317 KIRIMA SEC. SCHOOL CENTRE - P3672
KABUNGU SEC. SCHOOL - S4192 KIBO SEC. SCHOOL CENTRE - P0317 KIRINJIKO ISLAMIC SEMINARY - S0188
KABWE SEC. SCHOOL - S1848 KIBOGORA SEC. SCHOOL - S1458 KIRINJIKO ISLAMIC TEACHERS COLLEGE 


Link hii hufunguka kwa kasi sana.
Au


Jumatano, 28 Desemba 2016

Dhamana ya Mbunge Lema yagonga mwamba

Mbunge wa Arusha mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema amekosa dhamana baada ya mawakili wa upande wa Jamhuri kuweka pingamizi kukata rufaa.

Mawakili wa Godbless walikusudia leo Dessemba 28, kuwasilisha hoja sita mahakamani kwa kusudio la kutaka mteja wao apewe dhamana, lakini hali imekuwa tofauti baada ya Jamhuri kupinga rufaa hiyo.

Lema alikamatwa Novemba 2 mjini Dodoma, tangu wakati huo, ameshikiliwa katika gereza kuu la Kisongo jijini Arusha ambako amekaa kwa siku 56 sasa.

Baada ya kukamatwa mbunge huyo alifikishwa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, bwana Lema alipata dhamana na hakimu mkazi Desdery Kamugisha katika kesi namba 440 na 441/2016 akidaiwa kutoa lugha za uchochezi dhidi ya raisi wa awamu ya tano John Pombe Magufuli.

Cristiano Ronaldo ameshinda tuzo ya 9 kwa 2016

Mwanasoka wa wa kimataifa, Cristiano Ronaldo wa nchi ya Ureno, ambaye anachezea klabu ya mpira ya Raal Madrid ya Hispania anakamilsha mwaka wa 2016 kwa kushinda tuzo yake ya tisa.
Bwana Cristiano alifanikiwa  kushinda tuzo hiyo iliyojulikana kama Globe Soccer Award hapo Dubai.

Tuzo hii ya mkata kabumbu bora wa dunia (Globe Soccer Award) kwa mwaka huu wa 2016 imekuwa ni tuzo ya 9 kwa Cristiano kwa mwaka huu wa 2016, hii ni baada ya kujishindia tuzo kadha wa kadha, ikiwamo, The World Soccer Award, Four Four Two, Espy, Di Stéfano Award, Goal.com, FIFA Club Golden Ball, na Ballon d'Or.

Katika tuzo hiyo ya Globe Soccer Award 2016 aliyoibuka Ronaldo mshindi ilikuwa pia ikiwania na wachezaji kama Lionel Messi, Gonzalo Higuan, Antonie Griezmann, Jamie Vardy, mwanasoka huyu ameweza kushinda tuzo hizo kwa mara ya nne sasa, hii ni miaka tofauti ambayo amewvza pia kushinda tuzo hizi 2011, 2013 na 2014.

Hoja sita za Mbunge Godbles Lema kusikilizwa leo

Hoja sita za mawakili wa mbunge wa Arusha mjini (Chadema), Godbles Mlema kupinga kunyimwa dhamana zinatarajiwa kusikilizwa leo mbele ya mahakama kuu jijini Arusha.
Wakili Sheck Mfinanga anayemwakilisha Lema alisema waliwasilisha hoja hizo za rufaa kupinga uamuzi wa kunyimwa dhamana mteja wao.

Mbunge Lema anashikiliwa katika gereza kuu la Kisongo jijini Arusha tangu akamatwe Novemba 2 mwaka huu mjini Dodoma. Na sasa amekaa siku kwa 56.

Mara baada ya ya kukamatwa na kufikishwa mahakama ya hakimu mkazi Arusha, Lema alipewa dhamana na hakimu mkazi Desdery Kamughisha katika kesi namba 140 na141/ 2016 akidaiwa kutoa kauli za uchochezi dhidi ya raisi John Pombe Magufuli.

Hata hivyo, mkurugenzi wa mashitaka DPP alikata rufaa ya kupinga uamuzi wa mahakama kumpa dhamana Godbles Lema.

Hali imepelekea mawakili wa Lema nao kukata rufaa ya kupinga mteja wao kunyimwa dhamna, ili kesi isikilizwe tena leo baada ya kukwama kwa mda mrefu kutokana na kuwapo pingamizi nyingi za kisheria zilizowasilishwa na upande wa pili wa kesi (Jamhuri).










Jumamosi, 3 Desemba 2016

Baada ya Uchaguzi nchini Gambia, Barrow asema..

Baada ya uchaguzi nchini Gambia, raisi mteule wa nchi hiyo Bwana Adam Barrow amesema kuwa ni wakati wa kujenga Ghana yenye matumaini mpya.
Adama Barrow mwenye umri wa  miaka 51, na ambaye ni tajiri anayejishughulisha na biashara ya kujenga na kuuza majengo(nyumba), ameweza kushinda baada ya matokeo kutangazwa siku ya ijumaa na mkuu wa tume ya uchaguzi nchini Gambia, , Alieu Momarr Njai.

Barrow amemzidi Yahya kwa kura 51,416, ambapo kura za Barrow zilikuwa ni 263,515(45.5%) na Yahya kupata kura 212,099(36.7).

Raisi anayeachia madaraka nchini humo bwana Yaya Jammeh amekiri kushindwa, hii ni baada ya kumpigia Barrow na kumwahidi kumsaidia kujenga Gambia.


Yaya Jammeh ameweza kuingoza Gambia kwa miaka takribani 22, ambapo aliichukua nchi kwa mabavu na kujisimikia uongozi wa juu wa nchi ya Gambia(raisi).

Uchaguzi wa Gambia umewaacha wengi midomo wazi baada ya ushindi wa bwana Barrow kwa kile ambacho hakikutarajiwa, kwani Adam Barrow ni mgeni katika siasa na kwa upande wa Jammeh naye amekiri kushindwa jambo ambalo ni nadra kwa kiongozi mwenye tabia za kidikteta(mabavu).

Alhamisi, 24 Novemba 2016

Google, Facebook, Microsoft, Apple wavutiwa zaidi na roboti

Makampuni makubwa yanayotengeneza na kumiliki programu tofauti za kompyuta na simu, hivi karibuni yametangaza kuwa wamejikita katika ubunifu na uandaaji wa program roboti ambazo zitakazoweza kutumika katika kufanikisha kazi mbalimbali.


Kwa ujumla utengezaji wa roboti haujanza leo, ulianza mbali kuanzia miaka ya 1950 na 60. Na kwa wakati ule viliandaliwa pasipo ujengwaji mzuri wa grafiksi, japo ziliweza kuunganishwa katika mifumo ya kuratibu na kutoa huduma za mawasiliano ya papo(instant messaging services).


Kwa sasa zimeweza kuboreshwa pamoja na kuwa uweza wa kujibu maswali mbalimbali kwa watumiaji wake hasa kwa njia ya intaneti na kutoa majibu juu ya hayo maswali kwa njia iliyo sahihi.

Kwa nini Google, Facebook na Microsoft wavutiwe zaidi na utengezaji wa program roboti hizi..?

Haya makampuni yanaweza kufanya haya yote yakiwa na malengo mengi, haya ni baadhi tu:

 Kwa kufuata mahitaji ya watumiaji wake(wateja).
 Kwa kutaka kufanya mawasilano yawe mepesi na nafuu kwa watumiaji.
 Kuweza kutumika kama watoa huduma wa mwanzo kwa wateja kabla       mwanadamu hajahusishwa, na mwadamu atahusishwa endapo ufumbuzi         wa tatizo halijapatikana kwa msaada wa programu roboti.
  Programu hizi zinaweza kutumika zenyewe pasipo uendeshaji wa mtu, na                      kufanya huduma kuwa ya haraka na hakika hasa za kimwamala(benki) 

Apple ikiwa kama kampuni inayotengeneza vifaa vya teknolojia vitumiavyo umeme, kama vile simu, saa, kompyuta n.k wao wameweza kutengeneza programu roboti(Siri) ambayo hupatikana kwenye simu zao. Programu Siri, unaweza kumuuliza vitu ama ukamwomba aendeshe programu na akatoa majibu kulingana na maulizo yako, au akatoa mbadala wa kile unachokihitaji endapo kitakuwa hakipo.

Google nao wameweza kutengeneza programu roboti za namna tofauti, ikiwemo 
Google's web crawling bot (ama hufaamika kama "spider") ambayo huweza kukusanya taarifa kwa njia ya mtandao. Pia wamethubutu katika kutengeneza gari yenye uwezo wa kujiendesha yenyewe maarufu kama (Google Seft-Driving car).

Microsoft nao kwa sasa wanazo projekti nyingi wanazo shughulika nazo, lakini projekti yao maarufu ni ile programu roboti ijulikanayo kwa jina la 
Cortana, hii programu inapatikana kwenye programu yao kuu(os) kama vile Windows 10, Windows 10 Mobile, Windows Phone 8.1(windo toleo la kumi kwa kompyuta na simu na il ya toleo la 8.1)

Cortona inaweza kutoa majibu juu ya maswali yako kwa njia kuandika katika eneo la kuulizia (search engine) iwapo utakuwa umeunganisha kifaa(simu, komputa ama tableti-kibao) chako kwenye mtandao.

Facebook nao hawako nyuma, pia wamejikita zaidi katika kufanya tafiti maarufu kama 
Facebook AI Research (FAIR). Facebook wametengeneza vifaa maarufu kama vitual reality(ukweli uliotengenezwa) ambapo hii teknlojia imekusudiwa na facebook kutumika kwenye michezo ya gemu, kufanya mawasiliano ya kibishara, pamoja na kuona vitu ulivyonavyo mbali na kuhisi kama upo katika mazingira hayo. 

Mawasiliano yanayohusisha ujumbe wa papo(instant messaging) unaofanywa na makampuni kama WhatApp, Telegram, Hangouts, WeChat na Facebook messanger imepanuka kwa sasa na kuunganisha dunia kama kijiji.

Kumbe bi Hillary Clinton aliweza kushinda kwa kura nyingi.

Uchaguzi uliofanyika nchini Marekani wiki mbili zilizopita ambao ulishirikisha vyama kadha wa kadha, vikiwemo vyama viwili nguli, chama cha Republican kilichowakilishwa na bwana Donald Trump, na kile cha Democtrats ambapo wao walimsimisha bi Hillary Clinton kupeperusha bendera yake. 

Taarifa zimesema kuwa, kura za Clinton zimeongezeka mpaka milioni 2 kwa kura za kawahida. Japo katika huo uchaguzi wa Novemba 8, Trump alishinda kwa kuwa na kura nyingi za wajumbe,

Hivyo basi kwa sera na utaratibu wa nchi ya Marekani idadi kubwa ya kura za wajumbe ndizo huamua nani ni mshindi katika uchaguzi.

Hata hivyo baadhi ya watu wa kada mbalimbali wakiwemo wasomi, mawakili, na wanatakwimu wameweza kumshauri bi Clinton ili kuchungaza uhesabuji wa kura katika baadhi ya maeneo(majimbo) ambako kura ziliweza kupigwa na uhesabuji wake kufanyika kwa njia ya teknolojia ya komputa na ile ya kutumia njia ya desturi(makalatasi, kalamu, na skana).

Labda Clinton na timu yake itaweza kufanya hivyo kutokana na ushauri aliopata, japo kwa sasa hakuna lolote ambalo wameweza kulifanya.


MATOKEO YA URAISI kwa ujumla, kura zilizopigwa(%) na za wajumbE


Clinton 48.1% (232)Trump 46.6% (290)Johnson 3.3%Stein 1.0%
McMullin 0.4%









Democrats
Republican