Alhamisi, 24 Novemba 2016

Kumbe bi Hillary Clinton aliweza kushinda kwa kura nyingi.

Uchaguzi uliofanyika nchini Marekani wiki mbili zilizopita ambao ulishirikisha vyama kadha wa kadha, vikiwemo vyama viwili nguli, chama cha Republican kilichowakilishwa na bwana Donald Trump, na kile cha Democtrats ambapo wao walimsimisha bi Hillary Clinton kupeperusha bendera yake. 

Taarifa zimesema kuwa, kura za Clinton zimeongezeka mpaka milioni 2 kwa kura za kawahida. Japo katika huo uchaguzi wa Novemba 8, Trump alishinda kwa kuwa na kura nyingi za wajumbe,

Hivyo basi kwa sera na utaratibu wa nchi ya Marekani idadi kubwa ya kura za wajumbe ndizo huamua nani ni mshindi katika uchaguzi.

Hata hivyo baadhi ya watu wa kada mbalimbali wakiwemo wasomi, mawakili, na wanatakwimu wameweza kumshauri bi Clinton ili kuchungaza uhesabuji wa kura katika baadhi ya maeneo(majimbo) ambako kura ziliweza kupigwa na uhesabuji wake kufanyika kwa njia ya teknolojia ya komputa na ile ya kutumia njia ya desturi(makalatasi, kalamu, na skana).

Labda Clinton na timu yake itaweza kufanya hivyo kutokana na ushauri aliopata, japo kwa sasa hakuna lolote ambalo wameweza kulifanya.


MATOKEO YA URAISI kwa ujumla, kura zilizopigwa(%) na za wajumbE


Clinton 48.1% (232)Trump 46.6% (290)Johnson 3.3%Stein 1.0%
McMullin 0.4%









Democrats
Republican


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni