Alhamisi, 24 Novemba 2016

Google, Facebook, Microsoft, Apple wavutiwa zaidi na roboti

Makampuni makubwa yanayotengeneza na kumiliki programu tofauti za kompyuta na simu, hivi karibuni yametangaza kuwa wamejikita katika ubunifu na uandaaji wa program roboti ambazo zitakazoweza kutumika katika kufanikisha kazi mbalimbali.


Kwa ujumla utengezaji wa roboti haujanza leo, ulianza mbali kuanzia miaka ya 1950 na 60. Na kwa wakati ule viliandaliwa pasipo ujengwaji mzuri wa grafiksi, japo ziliweza kuunganishwa katika mifumo ya kuratibu na kutoa huduma za mawasiliano ya papo(instant messaging services).


Kwa sasa zimeweza kuboreshwa pamoja na kuwa uweza wa kujibu maswali mbalimbali kwa watumiaji wake hasa kwa njia ya intaneti na kutoa majibu juu ya hayo maswali kwa njia iliyo sahihi.

Kwa nini Google, Facebook na Microsoft wavutiwe zaidi na utengezaji wa program roboti hizi..?

Haya makampuni yanaweza kufanya haya yote yakiwa na malengo mengi, haya ni baadhi tu:

 Kwa kufuata mahitaji ya watumiaji wake(wateja).
 Kwa kutaka kufanya mawasilano yawe mepesi na nafuu kwa watumiaji.
 Kuweza kutumika kama watoa huduma wa mwanzo kwa wateja kabla       mwanadamu hajahusishwa, na mwadamu atahusishwa endapo ufumbuzi         wa tatizo halijapatikana kwa msaada wa programu roboti.
  Programu hizi zinaweza kutumika zenyewe pasipo uendeshaji wa mtu, na                      kufanya huduma kuwa ya haraka na hakika hasa za kimwamala(benki) 

Apple ikiwa kama kampuni inayotengeneza vifaa vya teknolojia vitumiavyo umeme, kama vile simu, saa, kompyuta n.k wao wameweza kutengeneza programu roboti(Siri) ambayo hupatikana kwenye simu zao. Programu Siri, unaweza kumuuliza vitu ama ukamwomba aendeshe programu na akatoa majibu kulingana na maulizo yako, au akatoa mbadala wa kile unachokihitaji endapo kitakuwa hakipo.

Google nao wameweza kutengeneza programu roboti za namna tofauti, ikiwemo 
Google's web crawling bot (ama hufaamika kama "spider") ambayo huweza kukusanya taarifa kwa njia ya mtandao. Pia wamethubutu katika kutengeneza gari yenye uwezo wa kujiendesha yenyewe maarufu kama (Google Seft-Driving car).

Microsoft nao kwa sasa wanazo projekti nyingi wanazo shughulika nazo, lakini projekti yao maarufu ni ile programu roboti ijulikanayo kwa jina la 
Cortana, hii programu inapatikana kwenye programu yao kuu(os) kama vile Windows 10, Windows 10 Mobile, Windows Phone 8.1(windo toleo la kumi kwa kompyuta na simu na il ya toleo la 8.1)

Cortona inaweza kutoa majibu juu ya maswali yako kwa njia kuandika katika eneo la kuulizia (search engine) iwapo utakuwa umeunganisha kifaa(simu, komputa ama tableti-kibao) chako kwenye mtandao.

Facebook nao hawako nyuma, pia wamejikita zaidi katika kufanya tafiti maarufu kama 
Facebook AI Research (FAIR). Facebook wametengeneza vifaa maarufu kama vitual reality(ukweli uliotengenezwa) ambapo hii teknlojia imekusudiwa na facebook kutumika kwenye michezo ya gemu, kufanya mawasiliano ya kibishara, pamoja na kuona vitu ulivyonavyo mbali na kuhisi kama upo katika mazingira hayo. 

Mawasiliano yanayohusisha ujumbe wa papo(instant messaging) unaofanywa na makampuni kama WhatApp, Telegram, Hangouts, WeChat na Facebook messanger imepanuka kwa sasa na kuunganisha dunia kama kijiji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni