Jumatatu, 21 Novemba 2016

Kiama Cha Vyuo Feki Nchini

Vyuo feki sasa kufutwa na Serikali.

Serikali ya Jamhuri ya Mhungano wa Tanzania imeweza kubaini uwepo wa vyuo vikuu lukuki ambavyo havina sifa.

Hivyo inakusudia kuvifuta hii ni kwa kutaka kuimarisha kiwango cha elimu inayotolewa na ngazi zote nchini.

Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia, Profesa Joyse Ndalichako ameyasma hayo jana siku ya jumatatu, Novemba 21, 2016, alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau wa elimu ya juu, jijini Dar-es-salaam.

Mheshimiwa waziri amesema hayo yamebainika baada ya jopo la wataalamu kufanya uhakiki humo vyuoni.

Profesa akasema, "Lengo ni kuhakikisha wasomi wanaohitimu kwenye vyuo hivyo, wanakuwa wameiva kitaaluma, ili pia waweza pia kushiriki katika kuijenga Tanzania ya viwanda".

Pia, Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya vyuo vikuu nchini(TCU) Profesa Jackobo Mtabaji, Amesema wamejipanga kuhakikisha kuwa wanafanya kazi zao kwa kusimamia mwongozo uliopo ili kuondoa mara moja huu uwepo wa vyuo vingi ambavyo havina sifa.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni